Mkulima

Mkulima I sell dogs, trained or untrained, wild or tame... The choice is yours. I also sell quail eggs and many other pets like monkey, tortoise and many more

UTENGENEZAJI WA CHAKULA CHA PEREGE/SATO WANAOKUZWA UTOMWILI(PROTEIN) 28%Dagaa                   18.25gUnga wa soya      ...
14/05/2019

UTENGENEZAJI WA CHAKULA CHA PEREGE/SATO WANAOKUZWA UTOMWILI(PROTEIN) 28%

Dagaa 18.25g
Unga wa soya 25g
Pumba za mpunga 6g
Unga wa muhogo 36.42g
Unga wa alizeti (mashudu) 10g
Vitamin-mineral mix 4.33g

UTENGENEZAJI WA CHAKULA CHA SAMAKI WAZAZI PEREGE(SATO) 44%

Dagaa 36.2g
Corn gluten meal 20.4g
Unga wa soya 17.7g
Copra meal 11.8g
Starch 3.2g
Cod liver oil 3.2g
Mafuta(vegetable oil) 0.5g
Vitamin-mineral mix 0.5g
Pumba za mchele 7.5g

Zingatia;
Lisha samaki wako katika eneo maalum na kwa wakati ule ule kilasiku. Hii itasaidia samaki wako kula chakula chote kwa sababu muda wa kula ukifika watakuwa katika eneo walilozoeshwa. Pia unaweza kuwafundisha samaki wako kula kwa mwitikio, yaani kabla ya kulisha gonga kengele au kitu chochote kinachoweza kutoa mlio kisha walishe. Fanya zoezi hili kila unapotaka kuwalisha hivyo watazoea.
Wakati unalisha anza kwa kiasi kidogo cha chakula na samaki wanapojaa katika eneo husika endelea kuongeza chakula hadi kiasi ulichopima kitakapoisha. Hakikisha ukubwa wa punje za chakula zinaendana na ukubwa / umri wa samaki. Kwa kawaida samaki wadogo hulishwa chakula cha unga na wakubwa hulishwa chakula cha punje(pellets).

VITU AMBAVYO MBWA HAPENDI KUFANYIWA.1. Kumshika kichwani. Mbwa sio paka, Hana jinsi kwasababu wewe ndo mmiliki wake. Mbw...
14/05/2019

VITU AMBAVYO MBWA HAPENDI KUFANYIWA.

1. Kumshika kichwani.
Mbwa sio paka, Hana jinsi kwasababu wewe ndo mmiliki wake. Mbwa anapenda kushikwa kwenye shingo, mgongoni na kifuani. Jiulize wewe unapenda kushikwa kichwani?

2. KUFUNGWA NA CHENI.
Mbwa hapendi kuvishwa cheni na kutembezwa barabarani, mzoeshe kutembea bila cheni ili awe huru kwasababu anafurahi kutembea na kunusa nusa vitu mbali mbali k**a kawaida yake.

3. KUELEKEZWA BILA VITENDO.
Mbwa ukimuelekeza bila kitendo au ukiwa unamuadhibu bila kitendo hakika atarudia kufanya vile vile. Hawezi kukuelewa kwa haraka unaongea nae nini.

4. KUMUOGESHA NA SABUNI ISIYO NA POVU JINGI.
Sio mbwa wote wanapenda maji kwahiyo povu jingi linamdanganya akubali kuoga, ukimaliza kumuogesha mchane kabla hajakauka kuondoa manyoya yanayotoka mwilini.

5. KURUSHA MDA WA KULA.
Ukimrusha mda wa kula ni k**a umemrusha mlo wake mmoja, hata wewe chai ukinywa saa 7 mchana itakuwa poa eeh?

Uzuri wa paka sio rangi.
12/05/2019

Uzuri wa paka sio rangi.

Ulishaji wa samakiUlishaji wa samaki hutegemea mambo mengi lakini kubwa ni kuwa chakula wanachokula huwa kinategemea uzi...
08/05/2019

Ulishaji wa samaki
Ulishaji wa samaki hutegemea mambo mengi lakini kubwa ni kuwa chakula wanachokula huwa kinategemea uzito walionao. Kwa kawaida samaki hula 5% ya uzito wake wa mwili akiwa mdogo na 3% akiwa mkubwa. Chakula anacholishwa na mfugaji huhesabika k**a cha ziada kutokana na ukweli kuwa, kill chakula cha asili tayari kinakuwa ndani ya maji. 5% ya uzito wa samaki inaweza kukadiriwa kwa kupima uzito wa kifaranga kimoja baada ya kuwa vimefika na kujua uzito wake na kisha kuuzidisha kwa idadi ya jumla ya vifaranga vilivyomo bwawani. Mfano k**a kifaranga kimoja kina gramu 100, 5% ya uzito huo ni gramu 5, zidisha kwa idadi ya vifaranga vyote ambayo inaweza kuwa vifaranga 1000, utazidisha 1000 mara 5 ambapo utapata gramu 5000 ambazo kilo 5 za chakula cha ziada utakachowalisha samaki wako.

Aina ya vyakula.
Sato wanaweza kulishwa mashudu ya pamba, pumba za mahindi, mashudu ya alizeti, mabaki ya dagaa, soya, karanga zilizosagwa, unga wa mahindi, unga wa mikate na mabaki ya vyakula k**a ugali.
Kuna mambo mengi sana ya kuzingatia unapoanza kufuga samaki, mambo mengine ni k**a vile kuzingatia miundo mbinu, wafanyakazi, kuzingatia masoko, utaalamu nk.

23/04/2019
Kwa wale wanaotaka kujua njia ya kutotolesha mayai kwa njia ya kienyeji nyumbani anifuate inbox nimpe maelekezo ni njia ...
12/04/2019

Kwa wale wanaotaka kujua njia ya kutotolesha mayai kwa njia ya kienyeji nyumbani anifuate inbox nimpe maelekezo ni njia fupi na nyepesi kufanya na mahitaji yake ni gharama nafuu. Kazi kwenu wafugaji, changamkia fursa hii.

06/04/2019

UFUGAJI WA KUKU NA SAMAKI KIBIASHARA.

UFUGAJI WA KUKU

Aina za KUKU.

Jinsi ya kufuga KUKU.

Utotoleshaji mayai.

Utamiaji wa asili na utotoleshaji vifaranga.

Utunzaji wa Banda na usafi.

Muhtasari juu ya utunzaji wa KUKU.

Magonjwa ya KUKU.

Magonjwa yatokanayo na lishe duni.

Malezi ya vifaranga kwa njia ya asili.

Namna ya kulea vifaranga vyenye umri wa siku moja hadi wiki nne kwa njia ya kisasa.

Maandalizi ya banda la kulelea vifaranga.

Jinsi ya kutengeneza kifaa cha kulelea vifaranga.

Usafi wa vyombo vya chakula na Maji.

Lishe ya KUKU na kuchanganya chakula.

Kuchanganya chakula cha KUKU.

Uwiano wa viinilishe vya chakula cha KUKU.

Namna ya kuchanganya chakula cha KUKU.

Mambo ya kuzingatia katika kulisha na kutunza chakula cha KUKU.

UFUGAJI WA SAMAKI KIBIASHARA

Aina za SAMAKI wanaofaa kufugwa.

SAMAKI aina ya Sato.

Mambo muhumi ya kuzingatia unapotaka kuanza kufuga samaki.

Eneo linalofaa kwa ufugaji wa SAMAKI aina ya Sato.

Mfugaji wa SAMAKI aepuke maeneo haya.

Namna ya kuandaa na kuchimba bwawa.

Aina za vyakula vya ziada vya SAMAKI.

Utunzaji wa bwawa na usafi.

Matatizo yanayoambatana na ufugaji wa SAMAKI.

Kwa vipengele hivyo hapo juu vya ufugaji wa kuku na samaki, k**a una swali, mchango au mtazamo wowote au k**a unahitaji maelezo kuhusu kipengele/vipengele chochote niandikie message na nitakujibu k**a unavyohitaji.

Wakulima wenzangu tupo pamoja kwenye kutafuta riski? Basi tushikane mikono na tuungane mikono tuwe kitu kimoja.

Foxy huyo buda full trained we tu
06/05/2017

Foxy huyo buda full trained we tu

Ulinzi muhimu. Tunalazimisha usalama.
14/11/2015

Ulinzi muhimu. Tunalazimisha usalama.

Singida mojaNamuita twiga mweupe.
14/11/2015

Singida moja
Namuita twiga mweupe.

Address

4948
Dar Es Salaam
255

Telephone

0784905061

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mkulima posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category